Featured Kitaifa

IGP WAMBURA ATETA NA BALOZI WA TZ NCHINI INDIA

Written by mzalendoeditor

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Camillus Wambura, leo 19 Oktoba 2022 ametembelea ofisi za ubalozi wa Tanzania uliopo nchini India na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania, Mhe. Anisa Mbega na kujadiliana mambo mbalimbali ikiwemo kutafuta fursa mbalimbali nchini humo hususani za kimasomo ili kuwezesha askari Polisi kufanya kazi kwa umahiri zaidi ikiwemo matumizi ya Sayansi na tekinolojia katika kuzuia uhalifu na wahalifu.

About the author

mzalendoeditor