Featured Kitaifa

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Prof. Mark James Mwandosya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).  Prof. Mwandosya anachukua nafasi ya Prof. Jamidu Hazzam Yahaya ambaye amemalizia muda wake.

Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Agosti, 2022.

Zuhura Yunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

About the author

mzalendoeditor