MABINGWA wa Zamani wa Ligi Kuu  Simba wameendeleza mwendo wa kugawa dozi baada ya kuichapa mabao 2-0 Mtibwa Sugar mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mchezo huo pia umetumika kumuaga beki Kisiki Paschal Wawa ambaye anamaliza mkataba wake na Simba.

Mabao ya Simba yamefungwa na Pape Sakho dakika ya 17 na bao la pili limefungwa na Peter Banda akipokea pasi kutoka kwa Pape Sakho

Kwa ushindi huo Simba wamefikisha Pointi 60 wakiendelea kubaki nafasi ya pili huku Mtibwa Sugar ikiwa nafasi ya 12 kwa Pointi 32 kila timu ikiwa imecheza mechi 28.

Previous article‘WADAU WA MAENDELEO TUUNGE KUDUMISHA MUUNGANO’:WAZIRI JAFO
Next articlePATA HABARI MOTO MOTO KATIKA MAGAZETI YA LEO JUNI 24,2022

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here