Featured Kitaifa

RAIS SAMIA AIAGIZA WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI KUZINGATIA MASHARTI YA MIKATABA KATIKA UJENZI WA BARABARA

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Nyahua-Chaya yenye 85.4 km zilizofanyika Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed SH. Albahar mara baada ya Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Nyahua-Chaya yenye 85.4 km zilizofanyika katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed SH. Albahar, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila, akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Barabara ya Nyahua-Chaya yenye 85.4 km katika Sherehe zilizofanyika Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed SH. Albahar wakizindua rasmi barabara ya Nyahua-Chaya 85.4 km kwenye Sherehe za ufunguzi wa barabara hiyo katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. Wengine katika picha ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani, pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed S. Albahar wakati akiwapungia mkono wananchi waliojipanga kando ya barabara ya Nyahua-Chaya mara baada ya ufunguzi uliofanyika katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. 

Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Nyahua-Chaya 85.4 km zilizofanyika katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei, 2022.

 *******************************

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa  Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuendelea kusimamia viwango vya ubora na kasi ya utekelezaji wa miradi kwa kuzingatia masharti ya Mikataba.

Rais Samia ametoa wito huo wakati akizindua barabara ya Nyahua- Chaya yenye urefu wa kilomita 85.4 iliyojengwa kwa ushirikiano na Mfuko wa Maendeleo wa Serikali ya Kuwait (KFAED) kwa gharama ya shilingi bilioni 123.9.

Aidha, Rais Samia amesema barabara hiyo ina umuhimu kwa kuwa inaunganisha kanda mbalimbali za nchi ikiwemo ukanda wa magharibi, wa kati, kaskazini, kusini, eneo la maziwa makuu pamoja na nchi za Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo kupitia Kigoma na Katavi.

Kwa upande mwingine, Rais Samia ametoa rai kwa wananchi kutokuhujumu miundombinu ya barabara pamoja na kuacha kutoa alama za barabarani kwa manufaa ya watumiaji kwa kuwa miundombinu hii inaigharimu Serikali fedha nyingi.

Rais Samia ameahidi kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Tabora ikiwemo kwenye sekta ya elimu, umeme, mawasiliano ya simu, soko la tumbaku pamoja na miundombinu ya barabara.

Awali, Mhe. Rais Samia alisimama na kuzungumza na wananchi wa eneo la Kigwa, Wilaya ya Uyui akiwa njiani kuelekea kijiji cha Tura kwa ajili ya uzinduzi wa Barabara hiyo.

About the author

mzalendoeditor