Featured Michezo

SIMBA YAICHAPA KIBABE BIASHARA UNITED LIGI YA NBC

Written by mzalendoeditor

Na Alex Sonna-DODOMA

MABIGWA watetezi Simba SC wameendelea kuifukuzia Yanga kimya kimya baada ya kupata ushindi wa kibabe wa mabao 3-0 dhidi ya Biashara United kutoka Mara Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Bara mchezo uliochezwa uwanja wa Benjamin Mkapa.

Simba walipata bao dakika ya 8 kupitia kwa  Pape Sakho aliyepokea pasi kutoka kwa Shomari Kapombe na kupiga  kiki kali akiwa nje ya boksi la 18 la Biashara na kuzama moja kwa moja nyavuni ilikimshinda kipa James Ssetuba.

Kiungo Mkabaji  Mzamiru Yassin aliwainua mashabiki wake baada ya kufunga bao la pili dakika ya 13 akiunganisha kwa kichwa mpira wa krosi uliopigwa na Kapombe.

Baada ya bao hilo, Simba iliendelea kuishambulia Biashara kwa nguvu na dakika ya 18 ilipata bao la tatu kupitia kwa Clatous Chama baada ya kupokea pasi ya Sakho akiwa ndani ya boksi la Biashara na kuwapiga chenga mabeki wawili waliolala chini kisha kupiga kiki ya wastani iliyoingia nyavuni.

Mnamo dakika ya 90 Simba walipata tuta baada ya Morrison kuangushwa ndani ya 18 na Meddie Kagere alikosa tuta hilo baada ya kipa James Ssetuba kiindaka hadi  mwamuzi wa kati Martin Sanya kutoka Morogoro anapuliza Kipyenga cha mwisho Simba wameibuka na ushindi wa mabao 3-0.

Kwa ushindi huo Simba wamefikisha Pointi 34 nafasi ya pili wakizidiwa Pointi 8 na Yanga wenye Pointi 42 huku Biashara United wakibaki nafasi ya 14 kwa Pointi 15.

Mchezo mwingine umechezwa uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba wenyeji Kagera Sugar wameshindwa kutamba katika uwanja wao baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Namungo FC kutoka Lindi

About the author

mzalendoeditor