Uncategorized

TCRA KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO KATIKA SEKTA HIYO NCHINI

Written by mzalendoeditor

MKURUGENZI  Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari,akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 leo Novemba 3,2022 jijini Dodoma.

……………………….

Na Alex Sonna-DODOMA

MKURUGENZI  Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Jabiri Bakari,amezitaja changamoto katika sekta hiyo nchini kuwa ni pamoja na uharibifu wa miundombinu ya mawasiliano.

Hayo ameyasema leo Novemba 3,2022 jijini Dodoma,wakati akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

“TCRA imendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kwenye kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda miundombinu ya mawasiliano”amesema Dkt.Bakari

Amesema, changamoto nyingine ni utoaji wa huduma za mawasilino kwa wote kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa bado.

Hata hivyo, amebainisha namna ambavyo wamekuwa wakikabiliana na kero hizo kupitia kituo cha kitaifa cha usalama mtandaoni (TZ-CERT) kimeendelea kukabiliana na uhalifu mtandaoni ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa wadau.

“TCRA imendelea kusimamia ubora wa huduma za mawasilinao kwa kutumia mitandao ya kisasa ili kuhakikisha huduma zinazaotolewa na watoa huduma zinakidhi viwango bora”amesema

Amesema kuwa TCRA inaendelea kuboresha na kusimamia kanuni za mawasiliano ya Kielectroniki na postal (Online Contents) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama vile Jeshi la Polisi,BASATA pamoja na Mahakama

Aidha amesema kuwa TCRA imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kama UCSAF, watoa huduma za mawasailianao ,Tanesco, Wakala wa umeme vijijini REA, Wakala wa Barabara vijijini (TARURA) pamoja na kuchangia katika mfuko wa mawasilinao kwa wote ili kuhakikisha kuwa huduma za  mawasailiano zinafika kwenye maeneo ambayo yajafikiwa.

Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa idara ya Habari -MAELEZO Gerson Msigwa,amesema kwa uwekezaji ambao serikali imeufanya katika sekta ya mawasiliano nchini hakuna mtu ambaye anaweza kufanya uharifu mtandaoni akabaki salama.

“Kwa namna ambavyo serikali hii ya awamu ya sita ilivyo wekeza katika sekta hii na vyombo vya dola vilivyo hakuna mtu anaweza kufanya uharifu akabaki salama watu wengi wanakamtwa sema ni huruma yetu lakini wakitaka ipo siku tutawataja unakuta wengine vijana wadogo tuu wanatumika kuituka serikali na viongozi wake”amesema Msigwa

MKURUGENZI  Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari,akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 leo Novemba 3,2022 jijini Dodoma.

MKURUGENZI  Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari,akisisitiza jambo kwa  waandishi wa habari (hawapo pichani) waliouliza maswali  kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 leo Novemba 3,2022 jijini Dodoma.

MSEMAJI Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa idara ya Habari -MAELEZO Gerson Msigwa,akizungumzia mambo mazuri yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita mara baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutoa taarifa kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 leo Novemba 3,2022 jijini Dodoma.

About the author

mzalendoeditor